Dawa Za UTI Za Hospital.

Matibabu ya UTI (Urinary Tract Infection) hutegemea aina ya maambukizi na hali ya mgonjwa.

Kwa kawaida, UTI husababishwa na bakteria, na dawa za hospitali zinazotumiwa hutegemea wingi wa maambukizi na vimelea vinavyohusika. 

uti

Zifuatazo ni baadhi ya dawa za kawaida zinazotumika kutibu UTI hospitalini:

1) Antibiotics Za Uti:

Antibiotics ni aina ya dawa zinazotibu maambukizi ya UTI kwa kuua bakteria wanaosababisha maambukizi. Baadhi ya antibiotics za kawaida zinazotumika kutibu UTI hospitalini ni pamoja na:

a) Nitrofurantoin (Macrobid, Macrodantin).

Hii ni moja ya dawa zinazotumika sana kutibu UTI, hasa kwa wanawake.

b) Trimethoprim/Sulfamethoxazole (Bactrim, Septra).

Mchanganyiko huu wa dawa ni maarufu kwa kutibu UTI zinazohusisha bakteria wengi.

c) Amoxicillin au Amoxicillin/Clavulanate (Augmentin).

Hii hutumika mara nyingi kwa maambukizi ya UTI yasiyo makali au kwa wajawazito wenye changamoto ya UTI.

d) Ciprofloxacin (Cipro) Na Levofloxacin (Levaquin).

Dawa hizi ni fluoroquinolones na hutumika kwa UTI kali au sugu.

e) Ceftriaxone.

Hii ni antibiotic ya sindano inayotumika kwa maambukizi makali ya UTI, hasa yanayoenea hadi kwenye figo.

f) Fosfomycin (Monurol).

Hii hutumika mara moja (single dose) kutibu maambukizi ya kibofu cha mkojo (cystitis).

2) Painkillers (Dawa Za Maumivu):

Kwa baadhi ya wagonjwa, maumivu yanayohusiana na UTI yanaweza kutibiwa na dawa za kupunguza maumivu kama vile:

a) Phenazopyridine (Pyridium).

Hii ni dawa ya kupunguza maumivu ya UTI, hususan maumivu wakati wa kukojoa, lakini haitibu maambukizi yenyewe.

b) Ibuprofen Au Paracetamol.

Hizi ni dawa za kawaida za maumivu ambazo zinaweza kusaidia kupunguza dalili za maumivu ya mgongo au tumboni inayohusiana na UTI.

3) Dawa Kwa Ajili Ya Maambukizi Sugu Au Makali:

Katika baadhi ya matukio ambapo UTI ni sugu au inahusisha figo (pyelonephritis), dawa zifuatazo zinaweza kutumika:

a) Gentamicin.

Hii ni antibiotic ya sindano inayotumika kwa maambukizi makali ya UTI.

b) Amoxicillin/Clavulanate (Augmentin).

Hii inatumika kutibu UTI sugu au maambukizi makubwa ya UTI.

c) Piperacillin/Tazobactam (Zosyn).

Hii hutumika kwa maambukizi makubwa zaidi ya UTI au kwa wagonjwa waliolazwa hospitalini.

Jinsi Ya Kuepuka Uti:

  • Kunywa maji mengi ili kusaidia kusafisha bakteria kutoka kwenye njia ya mkojo.
  • Kuepuka kukaa na mkojo kwa muda mrefu bila kukojoa.
  • Kujisafisha vizuri baada ya kujisaidia haja kubwa ili kuepuka kupeleka bakteria kutoka njia ya haja kubwa kwenda sehemu za siri. (Kwa wanawake)

Kumbuka:

Soma pia hizi makala:

Tahadhari:

Ni muhimu kwenda hospitali kwa uchunguzi wa kitaalamu, kwani dawa hizo hutolewa kulingana na uchunguzi wa daktari, na baadhi ya bakteria wanaweza kuwa sugu kwa aina fulani ya antibayotiki.