Madhara Ya Hormone Imbalance.

Hormone Imbalance Ni Nini?

Hormone imbalance ni hali ambapo kuna mabadiliko au kutokuwa na usawa katika viwango vya homoni mwilini. Homoni ni kemikali za mwili zinazosafirishwa kwa njia ya damu na kusimamia michakato mbalimbali mwilini, kama vile mzunguko wa hedhi, ukuaji, uzazi, na hisia.

Hormone imbalance inaweza kuwa na madhara mbalimbali kwa wanaume na wanawake, na madhara haya yanaweza kuathiri afya na ustawi wa mtu.

Hormone Imbalance

Madhara Ya Hormone Imbalance Kwa Wanaume:

Yafuatayo ni madhara ya hormone imbalance kwa wanaume ambayo ni pamoja na;

1) Kupungua Kwa Hamu Ya Kufanya Tendo La Ndoa.

Testosteroni ndicho kichocheo kikuu kinachodhibiti hamu ya tendo la ndoa kwa wanaume. Hvyo, wanaume wenye viwango vya chini vya testosteroni wanakabiliwa na kupungua kwa hamu ya kufanya tendo la ndoa, jambo linaloweza kuathiri mahusiano binafsi.

low sex drive in men

2) Kupungua Kwa Ubora Wa Shahawa.

Homoni za kiume, androgens zinadhibiti utengenezaji wa shahawa. Upungufu wa homoni hizi unaweza kusababisha kupungua kwa ubora wa shahawa, na hivyo kuathiri uzazi kwa wanaume.

low sperm count

3) Ukuaji Wa Matiti.

Homoni zisizo na usawa, hususan viwango vya chini vya testosteroni na ongezeko la homoni za kike kama estrojeni, zinaweza kusababisha ukuaji wa matiti kwa wanaume hali inayojulikana kama gynecomastia.

gynecomastia

4) Kupoteza Nywele.

Wanaume wenye testosteroni ya chini wanaweza kuanza kupoteza nywele au kupata upara haraka zaidi. Hii ni kutokana na athari za moja kwa moja za homoni kwenye foliko za nywele (hair follicles).

hairloss in men

5) Uchovu Wa Mara Kwa Mara.

Kama ilivyo kwa wanawake, wanaume wanaopata hormone imbalance wanaweza kuhisi uchovu wa mara kwa mara, ukosefu wa nishati, na kushindwa kuzingatia shughuli za kila siku.

depression

6) Mabadiliko Ya Hisia.

kama ilivyo kwa wanawake, hormone imbalance inaweza kusababisha wasiwasi, msongo wa mawazo, na mabadiliko ya ari (mood) kama vile huzuni, hasira.

mood swings in men

Madhara Ya Hormone Imbalalnce Kwa Wanawake:

Yafuatayo ni madhara ya hormone imbalance kwa wanawake ambayo ni pamoja na;

1) Kupungua Kwa Hamu Ya Tendo La Ndoa.

Homoni kama estrojeni, projesteroni, na testosteroni zinaathiri hamu ya tendo la ndoa. Kutokuwa na usawa wa homoni kunaweza kusababisha kupungua kwa hamu ya ngono, na pia inaweza kusababisha ukavu wa uke, hali inayofanya tendo la ndoa kuwa na maumivu.

low libido in woman

2) Mabadiliko Katika Mzunguko Wa Hedhi.

Hii ni mojawapo ya dalili kuu ya hormone imbalace kwa mwanamke. Hii inaweza kuwa mzunguko wa hedhi usio wa kawaida mfano kutokwa na damu nyingi au kidogo kuliko kawaida, au kutokuwepo kwa mzunguko wa hedhi kabisa.

Mabadiliko Katika Mzunguko Wa Hedhi

3) Ugumba.

Kutokuwa na usawa wa homoni za uzazi kunaweza kuathiri ovaries kutoa mayai (ovulation) na kufanya iwe vigumu kwa mwanamke kushika mimba (infertility). Homoni kama estrojeni na projesteroni zinadhibiti mzunguko wa hedhi, hivyo viwango visivyo vya kawaida vya homoni hizi vinaweza kuzuia uwezo wa kuzaa.

ugumba

4) Matatizo Ya Usingizi.

Kutokuwa na usawa wa homoni, hasa viwango vya chini vya projesteroni au estrojeni, kunaweza kuathiri usingizi. Hii inaweza kusababisha kukosa usingizi (insomnia), usingizi wa kusuasua, au hisia ya kuchoka baada ya kuamka.

insomnia

5) Kubadilika Kwa Ngozi Na Nywele.

Homoni huathiri afya ya ngozi na nywele. Kutokuwa na usawa wa homoni kunaweza kusababisha chunusi, ngozi kuwa kavu, nywele kunyonyoka, au nywele kuota sehemu zisizo za kawaida kama vile kwenye kidevu au kifua hali inayojulikana kama hirsutism.

hirsutism

6) Joto La Mwili Kubadilika.

Wanawake wanaopitia ukomo wa hedhi au wale wenye upungufu wa estrojeni wanaweza kuhisi joto la mwili kupanda ghafla (hot flashes) na jasho la usiku (night sweats), ambalo linaweza kusababisha usumbufu mkubwa na kuathiri usingizi.

hotflashes

Soma pia hii makala: Mambo 4 Muhimu Usiyo yajua Kuhusu Mvurugiko Wa Homoni Kwa Wanawake.

HITIMISHO:

Kuwasiliana na daktari ni muhimu ikiwa unakumbwa na dalili za hormone imbalance. Daktari anaweza kufanya vipimo vya damu na kutoa ushauri wa matibabu, kama vile tiba ya hormone (hormonal replacement therapy), mabadiliko ya mtindo wa maisha (lifestyle modification), au lishe bora ili kusaidia kurekebisha usawa wa hormone.