Jinsi Ya Kufanya Uume Uwe Imara.

Uume Imara (Afya Ya Uume):

Ili kufanya uume uwe imara (kuwa na nguvu wakati wa tendo la ndoa), unahitaji kuzingatia afya ya mwili, akili, na mtindo wa maisha.

uume

Zifuatazo ni baadhi ya njia muhimu na salama kabisa zinazosaidia uume uwe imara (kuwa na nguvu wakati wa tendo la ndoa);

1) Lishe Bora (Chakula Kina Nafasi Kubwa Sana).

Lishe bora ni msingi mkubwa wa afya ya uume kwa sababu  kusimama kwa uume (penile erection) hutegemea mtiririko mzuri wa damu.

Mwili unapopata virutubisho sahihi, huongeza mzunguko wa damu na uzalishaji wa homoni ya kiume, testosterone ambayo ni muhimu kwa nguvu za kiume.

Vyakula muhimu vya kuzingatia ni pamoja na;

a) Matunda kama tikiti maji, ndizi na parachichi – huongeza mzunguko wa damu

b) Mboga za majani (spinach, sukuma wiki) – zina nitrates zinazoongeza mtiririko wa damu

c) Samaki wenye mafuta (kama salmon, sardine) – wana omega-3 ambayo huimarisha afya ya moyo, kuongeza mtiririko wa damu kwenye mishipa ya damu

d) Karanga, ufuta, mbegu za maboga– zina madini ya zinki ambayo huongeza uzalishaji wa homoni ya kiume, testosterone

e) Kunywa angalau glasi 8–10 za maji kwa siku

Vyakula vya kuepuka ni pamoja na;

a) Vyakula vya mafuta mengi (fast food)

b) Vyakula vyenye sukari nyingi

 2) Fanya Mazoezi Ya Mwili Mara Kwa Mara.

Mazoezi ya mwili ni muhimu kwa kuboresha afya ya moyo na mzunguko wa damu, ambayo ni msingi wa afya uume wenye nguvu. Mazoezi ya mwili huongeza mtiririko wa damu kwenda kwenye uume, husaidia kupunguza mafuta mwilini ambayo yanaweza kuzuia mishipa ya damu. Lakini pia huongeza stamina na nguvu za mwili kwa ujumla.

Aina za mazoezi ya mwili unayoweza kufanya ni pamoja na;

  • Kukimbia au kutembea haraka
  • Kuruka kamba
  • Mazoezi ya viungo vya chini ya mwili (squat, lunges)
  • Mazoezi ya misuli ya nyonga (Kegel exercise)

3) Epuka Matumizi Ya Pombe Na Sigara Kupita Kiasi.

Pombe na sigara zina athari kubwa kwenye uwezo wa uume kusimama (erection) kwa sababu zinaathiri mzunguko wa damu, mfumo wa neva, na homoni iinayohusika na nguvu za kiume (testosterone).

Pombe Na Sigara

Kunywa pombe kupita kiasi kunaweza kuathiri afya ya uume kama ifuatavyo;

a) Hupunguza uwezo wa mfumo wa neva.

Uume husimama kutokana na ishara kutoka kwenye ubongo kwenda kwenye mishipa ya damu. Hivyo pombe hupunguza ufanisi wa mawasiliano haya ya neva, hufanya mwili ushindwe kuitikia msisimko wa kimapenzi kwa haraka.

b) Kupunguza mzunguko wa damu.

Uume unahitaji mzunguko mzuri wa damu ili kusimama. Pombe inasababisha mishipa ya damu kupanuka (vasodilation) kwa muda mfupi, lakini matumizi ya muda mrefu hupunguza ufanisi wa mishipa ya damu kwenye uume. Hii inaweza kusababisha tatizo la erectile dysfunction (ED), yaani kushindwa kusimama kwa uume.

c) Hushusha homoni ya kiume (testosterone).

Pombe inaweza kupunguza uzalishaji wa homoni ya kiume, testosterone, homoni muhimu kwa ajili ya hamu ya tendo la ndo kwa mwanaume  na nguvu ya uume. Hivyo kupungua kwa homoni hiyo kunasababisha kupungua hamu ya ngono na shida ya uume kusimama.

Sigara ina kemikali nyingi hatari, hasa nikotini, ambazo zinaathiri mishipa ya damu, hivyo matumizi ya sigara kupita kiasi huathiri afya ya uume kama ifuatavyo;

a) Husababisha mishipa ya damu kubana.

Nikotini husababisha mishipa ya damu kuwa myembamba (vasoconstriction). Hii inapunguza kiasi cha damu kinachofika kwenye uume.

b) Huharibu kuta za mishipa ya damu.

Hufanya mishipa kuwa migumu na isiyonyumbulika. Hii hupunguza uwezo wa mishipa kupanuka wakati wa msisimko.

c) Hupunguza oksijeni kwenye damu.

Moshi wa sigara una hewa ya kaboni monoksidi ambayo hupunguza hewa ya oksijeni kwenye damu hali ambayo huathiri afya ya uume kwani tishu za uume zinahitaji hewa ya oksijeni ya kutosha kufanya kazi vizuri.

d) Huongeza hatari ya magonjwa.

Sigara inahusishwa na magonjwa kama vile shinikizo la juu la damu (hypertension), magonjwa ya moyo ambapo magonjwa hayo yote yanaweza kuathiri moja kwa moja nguvu za uume.

4) Punguza Msongo Wa Mawazo (Stress).

Uume kusimama hutegemea ushirikiano kati ya ubongo, homoni, neva, na mzunguko wa damu.

Msongo Wa Mawazo (Stress)
.

Msongo wa mawazo huingilia mfumo huu kwa njia zifuatazo;

a) Huchochea homoni za stress (cortisol).

Wakati mwanaume ana msongo wa mawazo;

Mwili huzalisha cortisol kwa wingi. Cortisol ikitolewa kwa wingi hupunguza testosterone (homoni muhimu kwa hamu na nguvu za kiume).

Matokeo yake: Hamu ya tendo la ndoa hupungua na kusimama kwa uume kunakuwa dhaifu.

b) Huathiri mfumo wa neva.

Msongo wa mawazo huweka mwili katika hali ya “ kupigana (fight) or kukimbia (flight)”. Hali hii huzuia mwili kuwa na utulivu (relaxation),ambayo ni muhimu kwa uume kusimama. Hivyo ubongo hushindwa kutuma ishara sahihi za msisimko wa kimapenzi.

c) Huongeza mawazo ya hofu na wasiwasi.

Hofu ya kushindwa (performance anxiety) inaweza kufanya uume ushindwe kusimama.

Hii huunda mzunguko: hofu → kushindwa → hofu zaidi

d) Hupunguza mtiririko wa damu

Msongo wa mawazo unaweza kusababisha mishipa ya damu kubana, hali inayopelekea damu kutokutiririkai vizuri kwenda kwenye uume.

Kwa hiyo kupunguza msongo wa mawazo unashauriwa kulala vizuri, kufanya mazoezi ya kupumzika (meditation, kupumua kwa utulivu).

5) Dhibiti Uzito Wa Mwili.

Unene kupita kiasi unaweza kuathiri uzalishaji wa homoni ya kiume na mzunguko wa damu, hivyo kupunguza nguvu ya uume. Dhibiti uzito wa mwili kwa kufanya mazoezi ya mwili (physical exercises) mara kwa  mara kama vile kukimbia, kutembea haraka, kuruka kamba nk.

6) Pata Usingizi Wa Kutosha.

Usingizi mzuri (saa 6–8) husaidia homoni za mwili kufanya kazi vizuri, ikiwemo homoni ya kiume, testosterone. Uchovu unaweza kupunguza hamu na nguvu za tendo la ndoa.

7) Epuka Matumizi Ya Dawa Bila Ushauri Wa Dakari.

Dawa au virutubisho visivyo sahihi vinaweza kuathiri afya ya nguvu za kiume. Ni bora kupata ushauri wa daktari kabla ya kutumia dawa yoyote.

viagra

8) Dhibiti Magonjwa Sugu.

Magonjwa sugu kama vile kisukari, shinikizo la juu la damu, na unene kupita kiasi yanaweza kuathiri nguvu za kiume. Ni muhimu kuyadhibiti vizuri kwa  kupata ushauri wa daktari.

 kisukari, shinikizo la juu la damu,

HITIMISHO:

Kwa ujumla, uimara wa uume hutegemea zaidi afya ya mwili na mtindo wa maisha wa kila siku. Pale ambapo mwanaume anajitunza kupitia mazoezi, lishe bora, kupunguza msongo wa mawazo, kupata usingizi wa kutosha, na kuepuka tabia zinazodhuru mwili, uwezo wa mwili kufanya kazi vizuri huimarika, ikiwemo utendaji wa mfumo wa uzazi. Aidha, kudhibiti hali za kiafya na kutafuta msaada wa kitaalamu inapobidi husaidia kuhakikisha tatizo halizidi. Hivyo, kujenga na kudumisha afya bora kwa ujumla ndiyo msingi mkuu wa kuwa na uimara mzuri wa uume.

Dawa Ya Kuimarisha Misuli Ya Uume:

By the way, hivi unajua kwamba dawa ya asili iitwayo, PANACEA  itakusaidia kuimarisha misuli ya uume iliyolegea kutokana upigaji wa punyeto kiasi, matumizi ya pombe na sigara kupita kiasi? Ndiyo, kupata dawa hiyo wasiliana nasi kwa simu namba 0625 305 487, tunapatikana DODOMA mjini, Makulu center.