Sababu Za Kukosa Ute Ukeni.

Kukosa Ute Ukeni:

Kukosa ute ukeni ni tatizo ambalo linaweza kuathiri wanawake wengi na linaweza kusababishwa na mambo mbalimbali. 

ute ukeni

Sababu Za Mwanamke Kukosa Ute Ukeni:

Zifuatazo ni sababu zinazochangia mwanamke kukosa ute ukeni ambazo ni pamoja na;

1) Mabadiliko Ya Homoni.

Kupungua kwa viwango vya homoni, hususan estrogen, ni sababu kuu inayosababisha kukosa ute ukeni. Hali hii inaweza kutokea wakati wa kukoma hedhi, baada ya kuzaa, au wakati wa kunyonyesha.

homoni

2) Umri.

Kadri umri unavyoongezeka, wanawake wengi huanza kukutana na changamoto za kukosa ute.

Wanawake walio na umri wa miaka 20 hadi 28 wanaweza kupata ute wa uzazi kwa siku tano, wakati wale wenye umri wa miaka 30 hadi 40 wanaweza kuona kupungua kwa siku hizo.

3) Maambukizi Ukeni.

Maambukizi ya bakteria au fangasi kwenye uke yanaweza kusababisha ukavu ukeni. Maambukizi haya yanaweza kuleta dalili kama vile muwasho, kutokwa na uchafu ukeni, na maumivu wakati wa kujamiiana.

4) Matumizi Ya Dawa.

Baadhi ya dawa, kama vile zile za kutibu mzio (antiallergic drugs)), dawa za kuondoa msongo wa mawazo (antidepressant drugs), na dawa za kifafa (antiepileptic drugs), zinaweza kuathiri uzalishaji wa ute ukeni. Dawa za kupevusha mayai kama Clomid (clomiphene citrate) pia zinaweza kuchangia ukosefu wa ute.

5) Kusafisha Uke Kupita Kiasi.

Kusafisha uke mara kwa mara (excessive vaginal douching) kunaweza kuondoa bakteria wazuri katika uke (normal flora), hivyo kuongeza hatari ya maambukizi na kupunguza uzalishaji wa ute.

vaginal douching

6) Uzito Mdogo Kupita kiasi.

Wanawake wenye uzito mdogo sana au wanaofanya mazoezi makali wanaweza kuwa na kiwango kidogo cha estrogen, ambacho kinahitajika kwa uzalishaji wa ute ukeni.

7) Magonjwa Ya Zinaa.

Magonjwa ya zinaa (sexually transmitted diseases) kama vile kisonono na kaswende yanaweza pia kusababisha matatizo katika uzalishaji wa ute ukeni, ikiwa hayatatibiwa mapema.

Magonjwa ya zinaa

Matibabu Ya Kukosa Ute Ukeni:

Ili kutibu tatizo la kukosa ute ukeni, ni muhimu kuelewa chanzo chake. Mara nyingi, tiba inaweza kujumuisha:

  • Mabadiliko ya mtindo wa maisha (lifestyle modification).
  • Ushauri wa kitaalamu kutoka kwa daktari ili kubaini dawa sahihi.

Kuelewa sababu hizi kunaweza kusaidia wanawake katika kutafuta matibabu sahihi na kurejesha afya zao za uzazi.

Soma pia hii makala: Aina Za Ute Ukeni Na Maana Zake.

HITIMISHO:

By the way, hivi unajua kwamba dawa ya asili iitwayo PANACEA iliyotengenezwa kutokana na mimea na matunda yenye gharama ya TZS 85,000/= (dozi nzima ya wiki 2) itakusaidia kutatua changamoto ya kukosa ute ukeni?

panacea

Ndiyo ni kweli, kupata dawa hiyo wasiliana nasi kwa kubonyeza kitufe (button) kifutacho hapa chini, tunapatikana Dodoma mjini, majengo sokoni.